SlideShare une entreprise Scribd logo
1  sur  4
Télécharger pour lire hors ligne
Massamba na wenzake (2004). Wanasema,“fonolojia ni tawi la isimu ambalo
hujishughulisha na uchunguzi, uchambuzi na uainishaji wa sauti pambanuzi ambazo hutumika
katika mifumo mbalimbali ya sauti za lugha za binadamu.”
TUKI (2004) wanaifasili fonolojia kuwa ni tawi la isimu ambalo linajishughulisha na
uchambuzi wa mfumo wa sauti katika lugha.
Hivyo naweza kusema kuwa fonolojia ni utanzu wa Isimu unaochunguza jinsi sauti za
lugha zinavyofanya kazi katika lugha mahususi. Fonolojia hushughulikia jinsi sauti hizo
zinavyotumika, zinavyounganishwa na kupangwa katika lugha yoyote mahususi ili kuunda tungo
zenye maana. Kipashio cha msingi katika fonolojia ni fonimu na katika fonimu kuna konsonanti
na irabu.
Massamba na wenzake (2009) wanafasili mofolojia kuwa ni kiwango cha sarufi
kinachojishughulisha na uchambuzi wa mfumo wa maneno katika lugha yaani jinsi maneno ya
lugha yoyote iwayo inaundwa.
Besha (2007) anasema mofolojia ni taaluma inayojishughulisha na kuchambua muundo wa
maneno katika lugha. Misingi ya wataalamu hawa wawili wanaonekana kuingiliana katika
kuonyesha namna ya taaluma ya mofolojia inavyojihusisha na muundo wa maneno katika lugha.
Mofimu ndio kipashio cha msingi katika mofolojia.
Hivyo mofolojia inaweza kuelezwa kwamba ni taaluma inayoshughulika na uchunguzi na
uchambuzi wa maumbo mbalimbali ya maneno katika lugha.
UHUSIANO WA FONOLOJIA NA MOFOLOJIA
Ni kweli kimsingi taaluma ya mofolojia na fonolojia hufanana kwa kiasi kikubwa.
Kwanza, taaluma zote huhusika na uchunguzi na uchambuzi wa lugha za binadamu
sauti za lugha ni zile sauti zinazosaidia kujenga tungo zenye maana katika lugha. sauti za lugha
zinavyofuata mihimili katika kujenga tungo zenye maana katika lugha. Kuna uunganishaji wa
sauti kuunda silabi au mofimu, uunganisha wa mofimu kuunda maneno na maneno kuunda tungo
kubwa zaidi (sentensi). sauti za lugha ni sauti zenye kubeba maana na ambazo hutumiwa na
jamii fulani ya watu kwa madhumuni ya mawasiliano kati yao. Hii ina maana kuwa sauti za
lugha ya binadamu ama zinaweza kufanana sana au kwa kiasi fulani na pia zinaweza zikasigana
sana au kwa kiasi fulani tu.
Pili; vipashio vya kifonolojia ndivyo vinavyounda vipashio vya kimofolojia, kwa kutumia
fonimu ambacho ndio kipashio cha msingi katika fonolojia huweza kuunda mofimu ambayo
ndiyo kipashio cha msingi cha kimofolojia.
Mfano: /h/,/p/,/t/,/k/,/g/,/m/,/n/,/o/,/u/,/e/,/s/,/a/. fonimu hizo zinaweza kuunda mfuatano wa
maneno kama ifuatavyo.
kat-a = kata hivyo mfuatano wa fonimu /k/+/ a/ + /t/+ /a/ tumepata mofimu kata
pak-a = paka hivyo mfuatano wa fonimu /p/+/ a/ + /k/+ /a/ tumepata mofimu paka
nus-a = nusa hivyo mfuatano wa fonimu /n/+/ u/ + /s/+ /a/ tumepata mofimu nusa
Kutokana na mifano hii tumeweza kupata maumbo mbalimbali ya maneno kama vile kata, paka
na nusa ambayo ni maumbo ya kimofolojia.Hivyo ni dhahiri kwamba kuna uhusiano mkubwa
baina ya fonolojia na mofolojia.
Tatu; kanuni za kifonolojia zinaweza kutumika kuelezea maumbo ya kimofolojia .
Kanuni hizi si kwa kuelezea maumbo tu pia huweza kubadili umbo la neno yaani umbo la ndani
na umbo la nje. Kanuni hizo za kifonolojia ni udondoshaji, uyeyushaji, muungano wa sauti,
nazali kuathiri konsonanti, konsonanti kuathiri nazali na tangamano la irabu.
Udondoshaji, kanuni hii inahusu kuachwa kwa sauti fulani katika matamshi wakati
mofimu mbili zinapokaribiana yaani katika mazingira hayo hayo ya sauti ambayo ilikuwepo
hapo awali hutoweka.hapa kuangalia umbo la ndani la neno na umbo la nje. Umbo la ndani ni
jinsi neno lilivyoundwa na mofimu zake mbalimbali na umbo la nje ni jinsi neno lisikikavyo
linapotamkwa.
umbo la ndani umbo la nje
Muguu mguu
Mutu mtu
Mara nyingi irabu [u] katika mofimu “mu” inapokabiliana na mofimu fulani hasa konsonati
halisi katika mpaka wa mofimu, irabu [u] hudondoshwa lakini inapokabiliana na irabu
inayofanana nayo hubaki kama ilivyo. Kama vile Muuguzi-muuguzi Muumba- muumba
Uyeyushaji, hii ni kanuni inayohusu ubadilikaji wa irabu fulani kuwa nusu irabu au
viyeyusho ”. Viyeyusho vinavyohusika ni /w/ na /y/. kanuni hii hutokea katika mazingira
ambayo irabu [u] hukabiliana na irabu isiyo fanana nayo katika mpaka wa mofimu na kuwa /w/
lakini hubaki kama ilivyo mara ikabilianapo na irabu inayofanana nayo. Pia irabu [i] katika
mofimu inapokabiliana na irabu isiyofanana nayo hubadilika na kuwa /y/ katika mpaka wa
mofimu lakini hubaki kama ilivyo inapokabiliana na irabu inayofanana nayo.Mfano;
Mu+ema-----mwema Mu+ana-------mwana Mu+eupe-------mweupe Vi+ao------vyao
Muungano wa sauti, kanuni hii hutokea pale ambapo irabu ya mofimu moja
inapokabiliana na irabu ya mofimu nyingine katika mpaka wa mofimu irabu hizo huungana na
kuzaa irabu nyingine.
Mfano; Wa + ingi wengi, Ma + ino meno, Wa + izi wezi
Hivyo fonimu /a/ imeungana na fonimu /i/ na kubadilika na kuwa fonimu /e/ katika maneno
wengi, meno na wezi. Lakini kanuni hii haifanyi kazi wakati wote kwani kuna mazingira
mengine ambayo haifuati hasa katika mofimu mnyambuliko mfano; Wa +oko+a+ji -
waokoaji
Kwa kuhitimisha mofolojia na fonolojia zote ni nyanja za isimu zinazounda maarifa
fulani ya lugha kwa kuchunguza sauti na maumbo ya maneno yatokanayo na sauti za lugha hiyo
na mpangilio wake. Nyanja zingine za isimu ni kama fonetiki, sintaksia na semantiki. katika
Uundaji wa maneno au tungo zenye kuleta maana, fonolojia hushughulikia jinsi sauti hizo
zinavyotumika, zinavyounganishwa na kupangwa katika lugha yoyote mahususi ili kuunda tungo
zenye maana. Hivyo basi ili msemaji aweze kudhihirisha umilisi wake lazima aweze kupanga
vizuri konsonanti na irabu ili kuunda silabi. hiyo mofolojia huchunguza masuala kama vile aina
za mofimu, namna mofimu zinavyojenga maneno na namna mofimu zinavyohusiana ili kuunda
neno na lenye maana.
MAREJELEO
Besha, R.M. (2007). Utangulizi wa lugha na Isimu. Macmillan Aidan Ltd. Dar es Salaam.
Massamba, D.P.B. (2009). Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha. Taaasisi ya
Uchunguzi wa Kiswahili. Dar es salaam.
Massamba, D.P.B na wenzake. (2004). Fonolojia ya Kiswahili Sanifu. Taasisi ya
Uchunguzi wa Kiswahili. Chuo Kikuu cha Dar es salaam.
Mgullu, R.S. (1999). Mtalaa wa isimu: Fonetiki, Fonolojia na Mofolojia ya
Kiswahili. Longhorn publishers. Ltd. Nairobi.
CHUO KIKUU CHA MTAKATIFU AGUSTINO, TANZANIA
KITUO CHA BUKOBA
KITIVO CHA ELIMU
IDARA : KISWAHILI.
JINA LA KOZI: FONOLOJIA YA KISWAHILI.
MSIMBO WA KOZI: SW 211
JINA LA MHADHIRI: LUPAPULA, ABEL.
JINA LA MWANAFUNZI: MAPESA, NESTORY
NAMBA YA USAJILI : BAEDII 41584
AINA YA KAZI: KAZI BINAFSI.
TAREHE YA UWASILISHAJI: 16/12/2013
Swali;
Eleza kwa mifano uhusiano uliopo baina ya fonolojia na mofolojia.

Contenu connexe

Tendances

Chimbuko na Asili ya Kiswahili
Chimbuko na Asili ya KiswahiliChimbuko na Asili ya Kiswahili
Chimbuko na Asili ya Kiswahilimussa Shekinyashi
 
Utungaji wa kazi za fasihi
Utungaji  wa kazi za fasihiUtungaji  wa kazi za fasihi
Utungaji wa kazi za fasihiKAZEMBETVOnline
 
Lahaja za kiswahili kwa ujumla
Lahaja za kiswahili kwa ujumlaLahaja za kiswahili kwa ujumla
Lahaja za kiswahili kwa ujumlaWilson Pastory
 
KUKUA NA KUENEA KWA KISWAHILI
KUKUA NA KUENEA KWA KISWAHILIKUKUA NA KUENEA KWA KISWAHILI
KUKUA NA KUENEA KWA KISWAHILImussa Shekinyashi
 
Uhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishiUhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishiMussaOmary3
 
MAENDELEO YA KISWAHILI TANZANIA
MAENDELEO YA KISWAHILI TANZANIAMAENDELEO YA KISWAHILI TANZANIA
MAENDELEO YA KISWAHILI TANZANIAshahzadebaujiti
 
Kiswahili ni Pijini au Krioli
Kiswahili ni Pijini au KrioliKiswahili ni Pijini au Krioli
Kiswahili ni Pijini au Kriolimussa Shekinyashi
 
Kuongeza msamiati wa kiswahili
Kuongeza msamiati wa kiswahiliKuongeza msamiati wa kiswahili
Kuongeza msamiati wa kiswahiliKAZEMBETVOnline
 
Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihi
Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za FasihiUhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihi
Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihimussa Shekinyashi
 
Teaching Of Phonetics And Phonology At Ma Level In Pakistan
Teaching Of Phonetics And Phonology At Ma Level In PakistanTeaching Of Phonetics And Phonology At Ma Level In Pakistan
Teaching Of Phonetics And Phonology At Ma Level In PakistanDr. Cupid Lucid
 
Linguistics and the teacher
Linguistics and the teacherLinguistics and the teacher
Linguistics and the teacheryaseen zebary
 
Optimality theory.pptx
Optimality theory.pptxOptimality theory.pptx
Optimality theory.pptxamjadnaasir
 

Tendances (20)

MAENDELEO YA KISWAHILI
MAENDELEO YA KISWAHILIMAENDELEO YA KISWAHILI
MAENDELEO YA KISWAHILI
 
TAFSIRI NA UKALIMANI
TAFSIRI NA UKALIMANITAFSIRI NA UKALIMANI
TAFSIRI NA UKALIMANI
 
UTUMIZI WA LUGHA
UTUMIZI WA LUGHAUTUMIZI WA LUGHA
UTUMIZI WA LUGHA
 
Chimbuko na Asili ya Kiswahili
Chimbuko na Asili ya KiswahiliChimbuko na Asili ya Kiswahili
Chimbuko na Asili ya Kiswahili
 
Utungaji wa kazi za fasihi
Utungaji  wa kazi za fasihiUtungaji  wa kazi za fasihi
Utungaji wa kazi za fasihi
 
Lahaja za kiswahili kwa ujumla
Lahaja za kiswahili kwa ujumlaLahaja za kiswahili kwa ujumla
Lahaja za kiswahili kwa ujumla
 
KUKUA NA KUENEA KWA KISWAHILI
KUKUA NA KUENEA KWA KISWAHILIKUKUA NA KUENEA KWA KISWAHILI
KUKUA NA KUENEA KWA KISWAHILI
 
Tafsiri na ukalimani
Tafsiri na ukalimaniTafsiri na ukalimani
Tafsiri na ukalimani
 
Mjengo wa tungo 3
Mjengo wa tungo 3Mjengo wa tungo 3
Mjengo wa tungo 3
 
Uhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishiUhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishi
 
MAENDELEO YA KISWAHILI TANZANIA
MAENDELEO YA KISWAHILI TANZANIAMAENDELEO YA KISWAHILI TANZANIA
MAENDELEO YA KISWAHILI TANZANIA
 
Kiswahili ni Pijini au Krioli
Kiswahili ni Pijini au KrioliKiswahili ni Pijini au Krioli
Kiswahili ni Pijini au Krioli
 
UTUNGAJI
UTUNGAJIUTUNGAJI
UTUNGAJI
 
Kuongeza msamiati wa kiswahili
Kuongeza msamiati wa kiswahiliKuongeza msamiati wa kiswahili
Kuongeza msamiati wa kiswahili
 
Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihi
Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za FasihiUhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihi
Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihi
 
Uhifadhi wa fasihi simulizi
Uhifadhi wa fasihi simuliziUhifadhi wa fasihi simulizi
Uhifadhi wa fasihi simulizi
 
Teaching Of Phonetics And Phonology At Ma Level In Pakistan
Teaching Of Phonetics And Phonology At Ma Level In PakistanTeaching Of Phonetics And Phonology At Ma Level In Pakistan
Teaching Of Phonetics And Phonology At Ma Level In Pakistan
 
Linguistics and the teacher
Linguistics and the teacherLinguistics and the teacher
Linguistics and the teacher
 
Optimality theory.pptx
Optimality theory.pptxOptimality theory.pptx
Optimality theory.pptx
 
Phonology Introduction
Phonology IntroductionPhonology Introduction
Phonology Introduction
 

Plus de Mwl. Mapesa Nestory

Ge 249 research methods in geography by basheka J.J
Ge 249 research methods in geography by basheka J.JGe 249 research methods in geography by basheka J.J
Ge 249 research methods in geography by basheka J.JMwl. Mapesa Nestory
 
Ge 249 research methods in geography
Ge 249 research methods in geographyGe 249 research methods in geography
Ge 249 research methods in geographyMwl. Mapesa Nestory
 
Ge 249 SOPHISTS GROUP SAUT BUKOBA
Ge 249 SOPHISTS GROUP SAUT BUKOBA Ge 249 SOPHISTS GROUP SAUT BUKOBA
Ge 249 SOPHISTS GROUP SAUT BUKOBA Mwl. Mapesa Nestory
 
Water resources management river basin manage
Water resources management river basin manageWater resources management river basin manage
Water resources management river basin manageMwl. Mapesa Nestory
 
Powerpoint conjugaisons By Dr. Mapesa FRENCH NOTES
Powerpoint  conjugaisons By Dr. Mapesa     FRENCH  NOTESPowerpoint  conjugaisons By Dr. Mapesa     FRENCH  NOTES
Powerpoint conjugaisons By Dr. Mapesa FRENCH NOTESMwl. Mapesa Nestory
 
Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)
Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)
Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)Mwl. Mapesa Nestory
 

Plus de Mwl. Mapesa Nestory (9)

Ge 249 research methods in geography by basheka J.J
Ge 249 research methods in geography by basheka J.JGe 249 research methods in geography by basheka J.J
Ge 249 research methods in geography by basheka J.J
 
Ge 249 research methods in geography
Ge 249 research methods in geographyGe 249 research methods in geography
Ge 249 research methods in geography
 
Ge 249 SOPHISTS GROUP SAUT BUKOBA
Ge 249 SOPHISTS GROUP SAUT BUKOBA Ge 249 SOPHISTS GROUP SAUT BUKOBA
Ge 249 SOPHISTS GROUP SAUT BUKOBA
 
Water resources management river basin manage
Water resources management river basin manageWater resources management river basin manage
Water resources management river basin manage
 
Powerpoint conjugaisons By Dr. Mapesa FRENCH NOTES
Powerpoint  conjugaisons By Dr. Mapesa     FRENCH  NOTESPowerpoint  conjugaisons By Dr. Mapesa     FRENCH  NOTES
Powerpoint conjugaisons By Dr. Mapesa FRENCH NOTES
 
Basheka 244
Basheka 244Basheka 244
Basheka 244
 
Mapesa Nestory notes 1
Mapesa Nestory notes 1Mapesa Nestory notes 1
Mapesa Nestory notes 1
 
Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)
Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)
Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)
 
Rm 211
Rm 211Rm 211
Rm 211
 

Uhusiano fonolojia vs mofolojia

  • 1. Massamba na wenzake (2004). Wanasema,“fonolojia ni tawi la isimu ambalo hujishughulisha na uchunguzi, uchambuzi na uainishaji wa sauti pambanuzi ambazo hutumika katika mifumo mbalimbali ya sauti za lugha za binadamu.” TUKI (2004) wanaifasili fonolojia kuwa ni tawi la isimu ambalo linajishughulisha na uchambuzi wa mfumo wa sauti katika lugha. Hivyo naweza kusema kuwa fonolojia ni utanzu wa Isimu unaochunguza jinsi sauti za lugha zinavyofanya kazi katika lugha mahususi. Fonolojia hushughulikia jinsi sauti hizo zinavyotumika, zinavyounganishwa na kupangwa katika lugha yoyote mahususi ili kuunda tungo zenye maana. Kipashio cha msingi katika fonolojia ni fonimu na katika fonimu kuna konsonanti na irabu. Massamba na wenzake (2009) wanafasili mofolojia kuwa ni kiwango cha sarufi kinachojishughulisha na uchambuzi wa mfumo wa maneno katika lugha yaani jinsi maneno ya lugha yoyote iwayo inaundwa. Besha (2007) anasema mofolojia ni taaluma inayojishughulisha na kuchambua muundo wa maneno katika lugha. Misingi ya wataalamu hawa wawili wanaonekana kuingiliana katika kuonyesha namna ya taaluma ya mofolojia inavyojihusisha na muundo wa maneno katika lugha. Mofimu ndio kipashio cha msingi katika mofolojia. Hivyo mofolojia inaweza kuelezwa kwamba ni taaluma inayoshughulika na uchunguzi na uchambuzi wa maumbo mbalimbali ya maneno katika lugha. UHUSIANO WA FONOLOJIA NA MOFOLOJIA Ni kweli kimsingi taaluma ya mofolojia na fonolojia hufanana kwa kiasi kikubwa. Kwanza, taaluma zote huhusika na uchunguzi na uchambuzi wa lugha za binadamu sauti za lugha ni zile sauti zinazosaidia kujenga tungo zenye maana katika lugha. sauti za lugha zinavyofuata mihimili katika kujenga tungo zenye maana katika lugha. Kuna uunganishaji wa sauti kuunda silabi au mofimu, uunganisha wa mofimu kuunda maneno na maneno kuunda tungo kubwa zaidi (sentensi). sauti za lugha ni sauti zenye kubeba maana na ambazo hutumiwa na jamii fulani ya watu kwa madhumuni ya mawasiliano kati yao. Hii ina maana kuwa sauti za lugha ya binadamu ama zinaweza kufanana sana au kwa kiasi fulani na pia zinaweza zikasigana sana au kwa kiasi fulani tu. Pili; vipashio vya kifonolojia ndivyo vinavyounda vipashio vya kimofolojia, kwa kutumia fonimu ambacho ndio kipashio cha msingi katika fonolojia huweza kuunda mofimu ambayo ndiyo kipashio cha msingi cha kimofolojia. Mfano: /h/,/p/,/t/,/k/,/g/,/m/,/n/,/o/,/u/,/e/,/s/,/a/. fonimu hizo zinaweza kuunda mfuatano wa maneno kama ifuatavyo. kat-a = kata hivyo mfuatano wa fonimu /k/+/ a/ + /t/+ /a/ tumepata mofimu kata pak-a = paka hivyo mfuatano wa fonimu /p/+/ a/ + /k/+ /a/ tumepata mofimu paka nus-a = nusa hivyo mfuatano wa fonimu /n/+/ u/ + /s/+ /a/ tumepata mofimu nusa
  • 2. Kutokana na mifano hii tumeweza kupata maumbo mbalimbali ya maneno kama vile kata, paka na nusa ambayo ni maumbo ya kimofolojia.Hivyo ni dhahiri kwamba kuna uhusiano mkubwa baina ya fonolojia na mofolojia. Tatu; kanuni za kifonolojia zinaweza kutumika kuelezea maumbo ya kimofolojia . Kanuni hizi si kwa kuelezea maumbo tu pia huweza kubadili umbo la neno yaani umbo la ndani na umbo la nje. Kanuni hizo za kifonolojia ni udondoshaji, uyeyushaji, muungano wa sauti, nazali kuathiri konsonanti, konsonanti kuathiri nazali na tangamano la irabu. Udondoshaji, kanuni hii inahusu kuachwa kwa sauti fulani katika matamshi wakati mofimu mbili zinapokaribiana yaani katika mazingira hayo hayo ya sauti ambayo ilikuwepo hapo awali hutoweka.hapa kuangalia umbo la ndani la neno na umbo la nje. Umbo la ndani ni jinsi neno lilivyoundwa na mofimu zake mbalimbali na umbo la nje ni jinsi neno lisikikavyo linapotamkwa. umbo la ndani umbo la nje Muguu mguu Mutu mtu Mara nyingi irabu [u] katika mofimu “mu” inapokabiliana na mofimu fulani hasa konsonati halisi katika mpaka wa mofimu, irabu [u] hudondoshwa lakini inapokabiliana na irabu inayofanana nayo hubaki kama ilivyo. Kama vile Muuguzi-muuguzi Muumba- muumba Uyeyushaji, hii ni kanuni inayohusu ubadilikaji wa irabu fulani kuwa nusu irabu au viyeyusho ”. Viyeyusho vinavyohusika ni /w/ na /y/. kanuni hii hutokea katika mazingira ambayo irabu [u] hukabiliana na irabu isiyo fanana nayo katika mpaka wa mofimu na kuwa /w/ lakini hubaki kama ilivyo mara ikabilianapo na irabu inayofanana nayo. Pia irabu [i] katika mofimu inapokabiliana na irabu isiyofanana nayo hubadilika na kuwa /y/ katika mpaka wa mofimu lakini hubaki kama ilivyo inapokabiliana na irabu inayofanana nayo.Mfano; Mu+ema-----mwema Mu+ana-------mwana Mu+eupe-------mweupe Vi+ao------vyao Muungano wa sauti, kanuni hii hutokea pale ambapo irabu ya mofimu moja inapokabiliana na irabu ya mofimu nyingine katika mpaka wa mofimu irabu hizo huungana na kuzaa irabu nyingine. Mfano; Wa + ingi wengi, Ma + ino meno, Wa + izi wezi Hivyo fonimu /a/ imeungana na fonimu /i/ na kubadilika na kuwa fonimu /e/ katika maneno wengi, meno na wezi. Lakini kanuni hii haifanyi kazi wakati wote kwani kuna mazingira mengine ambayo haifuati hasa katika mofimu mnyambuliko mfano; Wa +oko+a+ji - waokoaji Kwa kuhitimisha mofolojia na fonolojia zote ni nyanja za isimu zinazounda maarifa fulani ya lugha kwa kuchunguza sauti na maumbo ya maneno yatokanayo na sauti za lugha hiyo na mpangilio wake. Nyanja zingine za isimu ni kama fonetiki, sintaksia na semantiki. katika Uundaji wa maneno au tungo zenye kuleta maana, fonolojia hushughulikia jinsi sauti hizo zinavyotumika, zinavyounganishwa na kupangwa katika lugha yoyote mahususi ili kuunda tungo zenye maana. Hivyo basi ili msemaji aweze kudhihirisha umilisi wake lazima aweze kupanga vizuri konsonanti na irabu ili kuunda silabi. hiyo mofolojia huchunguza masuala kama vile aina za mofimu, namna mofimu zinavyojenga maneno na namna mofimu zinavyohusiana ili kuunda neno na lenye maana.
  • 3. MAREJELEO Besha, R.M. (2007). Utangulizi wa lugha na Isimu. Macmillan Aidan Ltd. Dar es Salaam. Massamba, D.P.B. (2009). Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha. Taaasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. Dar es salaam. Massamba, D.P.B na wenzake. (2004). Fonolojia ya Kiswahili Sanifu. Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. Chuo Kikuu cha Dar es salaam. Mgullu, R.S. (1999). Mtalaa wa isimu: Fonetiki, Fonolojia na Mofolojia ya Kiswahili. Longhorn publishers. Ltd. Nairobi.
  • 4. CHUO KIKUU CHA MTAKATIFU AGUSTINO, TANZANIA KITUO CHA BUKOBA KITIVO CHA ELIMU IDARA : KISWAHILI. JINA LA KOZI: FONOLOJIA YA KISWAHILI. MSIMBO WA KOZI: SW 211 JINA LA MHADHIRI: LUPAPULA, ABEL. JINA LA MWANAFUNZI: MAPESA, NESTORY NAMBA YA USAJILI : BAEDII 41584 AINA YA KAZI: KAZI BINAFSI. TAREHE YA UWASILISHAJI: 16/12/2013 Swali; Eleza kwa mifano uhusiano uliopo baina ya fonolojia na mofolojia.